Advertisements

Sunday, February 28, 2010

Ramsey afanyiwa upasuaji kuunga mguu




 Kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey amefanyiwa upasuaji kuunga sehemu ya chini ya mguu wake wa kulia uliyovunjika baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Stoke siku ya Jumamosi.
Ramsey mwenye umri wa miaka 19 anayechezea pia timu ya taifa ya Wales alitolewa nje ya uwanja kwa machela baada ya kuchezewa rafu na mlinzi wa Stoke Ryan Shawcross, aliyetolewa nje kwa kadi nyekundu huku akibubujikwa na machozi akijutia kosa hilo.
Taarifa iliyotolewa na klabu ya Arsenal kupitia mtandao wake imesema upasuaji aliofanyiwa Ramsey siku ya Jumamosi ulikwenda vizuri, lakini hajafahamika lini atapona kabisa.
Kwa muda uliosalia kumalizika msimu huu Ramsey hataweza kucheza soka.
Baada ya mchezo wa siku ya Jumamosi, meneja wa Arsenal, Arsene Wenger ameielezea rafu aliyochezewa Ramsey "haukubaliki kabisa".
Lakini baadae Shawcross alielezea masikitiko yake kwa Ramsey na akasema katika taarifa yake rasmi, hakukusudia kumuumiza kwa makusudi kutokana na rafu aliyocheza.
Ameongeza kusema: "Kamwe sina tabia ya kumuumiza mchezaji mwenzangu. Nimeuzunishwa Aaron ameumia vibaya na ninamuombea apone haraka"
Pata kideo jinsi alivyoumia.

Tenerife 1 - 5 Real Madrid

Real Madrid forward Gonzalo Higuain celebrates after scoring against Tenerife at the Heliodoro Rodriguez Lopez Stadium on Saturday.
Real Madrid foward Gonzalo Higuan celebrates after scoring agaist Tenerife at the Helodoro Rodriguez Lopez stadium on saturday

John F Kitime na Anania U.S.A. Tour 2010


John Kitime akiwa na Anania Connecticut,alhamisi picha kwa hisani ya Issack Kibodya

Mdau Issack Kibodya akielekea Connecticut

Mzee Mwendamani kulia nae alikukua miongoni mwa wabongo walioenda Connecticut

Hitma ya Balozi Daudi Mwakawago,Boston Massachusetts

Liverpool 2 - 1 Blackburn

Steven Gerrard celebrates putting Liverpool in front
Reds skipper Gerrard scored against the run of play at Anfield

Aston Villa 1 - 2 Man Utd

Wayne Rooney started on the bench but finished as the hero
Rooney started on the bench but finished as the game's match-winner

zimebaki kama wiki tatu,kijua kichomoze ughaibuni


inapoanza Spring Break shughuli za BBQ hua kila kona

harlie Sheen's Ex: He Pushed, Threatened to Kill

Denise Richards 
The D.A. in Aspen may call Charlie Sheen's ex-wife, Denise Richards, to testify about an alleged incident that is eerily similar to the allegations of his current wife, Brooke Mueller.

We're told the Pitkin County D.A. has had law enforcement in L.A. County contact Richard's agent and lawyer, about Denise possibly testifying in Charlie Sheen's criminal case in Aspen. Specifically, sources tell us the D.A. is interested in a declaration Denise signed
 under penalty of perjury in 2005, when she got a restraining order against the "Two and a Half Men" star.

Richards claimed on December 30, 2005, in the middle of an argument, she was holding their daughter Lola, when Charlie "pushed me, shoving me with his two hands between my shoulders. I was forced backwards and tripped over one of the children's toys and fell on the floor with Lola."

According to the declaration, Charlie then pointed his finger at her and screamed, "I hope you f--king die, bitch." Richards says as Charlie was walking out the front door
 he said "he was going to have me killed. He said you are f--king with the wrong guy."


Iraq kuwarejesha kazini wanajeshi 20,000 waliokua chini ya Saddam Hussein

An Iraqi soldier stands guard at a polling station in Basra ahead of the March 7 general elections.
Waziri mkuu wa Iraq Nuri al-Maliki,anafikiria kuwarejesha kazini wanajeshi takriban 20,000 waliokua chini ya utawala wa Saddam Hussein 

Rwanda yamfuta balozi wake wa India



Balozi wa Rwanda nchini India, Lt. Jenerali. Kayumba Nyamwasa, ameng'atuka katika nafasi yake na kuvuliwa wadhifa huo na serikali ya Rwanda.
Jenerali Nyamwasa, ambaye ni kamanda wa zamani wa kundi la waasi nchini Rwanda lililotwaa madaraka mwaka wa 1994, anaarifiwa kuwasili nchini Uganda.
Serikali ya Rwanda imesema kamanda huyo wa zamani alihojiwa na maafisa wa upepelezi wa makosa ya jinai baada ya kurejea mjini Kigali kwa mashauriano.
Serikali ya Rwanda sasa inataka afisa huyo arejeshwe kutoka Uganda.
Jenerali Nyamwasa ni mwanadiplomasia wa pili wa Rwanda kuachia ngazi katika majuma ya hivi karibuni.

Capello: Terry hatakuwa nahodha chini yake


Kocha wa England Fabio Capello amesema John Terry kamwe hatorejea kuwa nahodha wa timu hiyo chini ya uongozi wake.
Terry alivuliwa unahodha baada ya tuhuma zinazohusu maisha yake binafsi huku Rio Ferdinand akichukua nafasi yake.
Capello amesema hadi katika Kombe la Dunia, Terry hatakuwa nahodha tena. Baada ya Kombe la dunia, iwapo atendelea kuwa kocha wa England pia hadhani kama Terry ataweza kuwaongoza wenzake.
Ameongeza kusema Capello, "ninataka nahodha kuwa mfano mzuri kwa vijana wadogo. Kile alichofanya sio kizuri, nimemueleza hilo na ameelewa."
Terry, mwenye umri wa miaka 29, bado ana imani atarejea katika nafasi yake ya unahodha, lakini Capello anahisi hafai tena kuwa nahodha kutokana na kumuendea kinyume mchezaji mwenzake wa England Wayne Bridge.

Tetemeko lauwa zaidi ya mia tatu Chile


Rescue team in Concepcion Rais wa Chile, Michelle Bachelet, amesema watu wapatao millioni mbili wameathiriwa na tetemeko kubwa la ardhi lililotokea nchini humo siku ya Jumamosi.
Zaidi ya watu mia tatu wamethibitishwa kufariki dunia katika janga hilo.
Tetemeko hilo lenye kiwango cha 8.8 katika vipimo vya majanga hayo, lilisababisha mawimbi ya tsunami katika eneo nzima la Pacific, ingawa mawimbi hayakuwa makubwa kama ilivyotabiriwa hapo awali.
Ni tetemeko kubwa zaidi kutokea Chile katika kipindi cha miaka hamsini.
Uharibifu mkubwa wa barabara na majengo umeripotiwa katika maeneo mengi, ukiwemo mji mkuu, Santiago, ambako kiwanda cha kemikali kilishika moto.
Hakuna huduma muhimu kama vile mawasiliano ya simu, maji na umeme.
Picha za televisheni zilionyesha daraja kubwa mjini Concepcion ambalo lilianguka katika mto wa Biobio, huku makundi ya waokoaji yakiendelea kuwatafuta manusura katika majengo yaliyoanguka.
Wafungwa zaidi ya mia mbili nawo waliweza kutoroka jela katika mji wa Chillan, lakini 60 kati yao walikamatwa tena na vikosi vya usalama.
Rais Barack Obama alisema Marekani iko tayari kutoa msaada iwapo serikali ya Chile itatoa ombi rasmi.

TAMASHA LA MUZIKI LAFANA,BETHESDA,MARYLAND

watu wengi walihudhulia tamasha

Rev Baraza alikonga nyoyo za mashabiki
Aj Ubao  mwenye miwani naye alikuwepo kwenye Tamasha kama mgeni mualikwa,AJ UBAO ANATISHA!!!!!!

Saturday, February 27, 2010

Kisomo cha Baba yake dada Aisha Bwalu,Dc

Sheh Dullah wa pili kushoto naye alikuwepo kwenye kisomo cha Baba yake Aisha Bwalu

Bwalu kati(T-Shati nyekundu) akiwa na ndugu na jamaa waliofika kwenye kisomo

Dj Rich kulia na Francis Makala watatu kushoto kutoka Massachusetts nao walikuwepo
Dada zetu wa Dc nao walikuwepo kwenye kisomo
wakina mama nao walijumuika pamoja

Rooney huenda akapumzika Kombe la Carling


Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson anafikiria kumpumzisha mshambuliaji wake hatari Wayne Rooney katika mchezo wa fainali ya Kombe la Carling na Aston Villa.
Rooney tayari amekwishapachika mabao 11 katika michezo minane iliyopita, lakini Ferguson anapima iwapo mshambuliaji huyo anahitaji kupumzika au la.
Ferguson amesema bado anafikiria. Tatizo Rooney anahitaji kucheza kila mechi.
United wiki mbili zijazo watakabiliana na AC Milan katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na pia wanajinoa kwa ajili ya kutetea taji la Ligi Kuu ya England wakichuana na Chelsea.
Ferguson anakabiliwa na kibarua kigumu kuchagua timu kwa ajili ya mechi na Aston Villa, ambao wanakiu ya kumaliza ukame wa miaka 14 bila ya kombe.

Stoke 1 - 3 Arsenal

Ryan Shawcross
Ryan Shawcross leaves the pitch in tears after his challenge on Ramsey

Galliani pins his faith in Leonardo

Leonardo: Has VP's backing 
                        Leonardo has VP'Sbacking


AC Milan vice-pesident Adriano Galliani has thrown his support behind Leonardo as they bid to keep the pressure on Inter Milan this weekend.

Only a few weeks ago, Leonardo's position was being openly questioned by club owner Silvio Berlusconi, but since then Milan have closed the gap to Inter to four points, aided by the dramatic midweek come-from-behind victory over Fiorentina.

Galliani claimed Berlusconi called him after that match to praise the players and the coach for the manner of the victory.

"The president called me after the match in Florence to say that we have a great goalkeeper," he said. "We have Ronaldinho, a great player. And do you see the confidence is paying off?

Ofisi ya ubalozi wa Tanzania nchini Marekani kuhamia rasmi jengo jipya Jumatatu

mjengo mpya wa ofisi za ubalozi wa Tanzania Marekani zilizopo 1232 22 St,Nw,Washington,Dc ambao utaanza kutumiwa rasmi Jumatatu march 1,2010


mjengo wazamani wa ofisi ya ubalozi wa Tanzania uliokua R St,Nw,Dc  

BUNDI AMEINGIA DARAJANI




Home TeamScoreAway TeamTime
Chelsea2-4Man City
(HT 1-1)
  • Lampard 42
  • Lampard (pen) 90+1
  • Tevez 45+1
  • Bellamy 51
  • Tevez (pen) 76
  • Bellamy 87

Nigeria yampata Msweden Lagerback


 Nigeria imemteua kocha wa zamani wa Sweden Lars Lagerback kuwaongoza katika Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini mwezi wa Juni.
Lagerback aliteuliwa akiwa amewapiku Glenn Hoddle na Sven-Goran Eriksson, ambao wote walikuwa waiinyemelea kazi hiyo.
Msemaji wa Shirikisho la Soka la Nigeria Ademola Olajire amesema Hoddle na kocha wa zamani wa Senegal Bruno Metsu waliwavutia wakati wa mahojiano.
Lakini akaongeza Lagerback kwa sasa amekwishatia saini mkataba wa miezai mitano kuifundisha Nigeria kuelekea katika Kombe la dunia.

Tetemeko kubwa latokea Chile

mmoja wa watu waliojeruhiwa katika tetemekoWatu kumi na sita wanaarifiwa kufariki dunia kufuatia temeko kubwa la ardhi lililo na kiwango cha takriban alama tisa katika vipimo vya matetemeko ya ardhi nchini Chile.
Tetemeko hilo linasemekana kuwa la nguvu zaidi kuwahi kutokea nchini humo.
Watu katika mji mkuu Santiago, zaidi ya kilomita mia tatu kutoka katika kitovu cha tetemeko hilo wameelezea kuamshwa na mtikisiko huo ulioangusha vyombo na meza.
Nyaya za simu na umeme pia ziliharibika.
Rais wa Chile, Michelle Bachelet, amesema kuwa idadi ya vifo inaweza kuongezeka huku watu wakishauriwa kubaki nyumbani.
Idara ya Marekani inayotoa tahadhari kuhusu matetemeko, imesema kiwango cha bahari kilionyesha ishara za tsunami, lakini haikuweza kupata ufafanuzi juu ya ukubwa wake.
Tetemeko hilo pia lilisikika katika maeneo ya Andes nchini Argentina.

Friday, February 26, 2010

Tamasha La Muziki,HAKUNA KIINGILIO

Tamasha la muziki wa Afrika Rev Baraza akishirikiana na mshindi wa Kora Award George Okudi na Aj Ubao na wengineo leo jumamosi feb 27 2010 
address 5033 Wilson Lane,
Bethesda,Md,20814

VINYWAJI NA VITAFUNIO NI BURE
PARKING KIBAO NA BURE

Kuanzia saa 10 jioni(4pm) mpaka saa 4 usiku(10pm)

Ajali ya meli Misri yaua watatu


3 die in Cruise liner smash
Maafisa wamesema, meli ya kifahari imegonga gati katika hoteli ya Misri Sharm al-Sheikh, na kusababisha vifo vya mabaharia watatu.
Takriban watu wengine wanne wamefariki dunia wakati meli hiyo ya Costa Europa, iliyobeba abiria 1,473, ilipofika kwenye bandari baada ya hali ya hewa kubadilika.
Mamlaka ya bandari ya bahari ya Sham imesema mabaharia waliokufa ni kutoka India, Honduran na Brazil.
Walioripotiwa kujeruhiwa ni wawanwake watatu raia wa Uingereza na mmoja kutoka Italia.

24 wafa Timbuktu


A picture taken on April 10, 2006 shows the Djinguereber mosque of Timbuktu, where a stampede left at least 24 people crushed to death and many more injured, officials and witnesses said on February 26, 2010.
picha ya msikiti ulioanguka Djinguereber Timbuktu na kuuwa watu wanaokadiriwa 24,picha hii ilipigwa april 10 2006

 Takriban watu 24, wengi wakiwa wanawake na watoto, wamefariki dunia kutokana na msongamano katika msikiti maarufu wa Djinguereber huko Timbuktu.
Mtafaruku huo ulitokea katika sherehe za Maulid kuadhimisha kuzaliwa kwa mtume Muhammad, wakati watu walipouzunguka msikiti huo uliotengenezwa kwa tope kaskazini mwa Mali.
Waumini walitumia njia tofauti na walioizoea kutokana na kufanyiwa ukarabati wa jengo hilo lililojengwa tangu karne ya 14.
Timbuktu, iliyopo katika jangwa la Sahara, zamani ilikuwa kituo cha mafunzo ya kiislamu.
Ripoti moja inasema tukio hilo limetokea wakati mama mmoja mtu mzima alipoanguka huku maelfu wengine wakijaribu kuzunguka msikiti huo mara tatu.

SABORES LOUNGE,3435B CONNECTICUT AV,NW,WASHINTON,DC,20008


 
LUKE MUSIC FACTORY,
invites you tonight Feb 27 at Sabores Lounge from 10:30pm,Music By Dj Luke Feat Dj Kay,BEST PLACE TO MENGLE WITH YOUR FRIENDS
no cover charge
PARK AT THE METRO

               KISOMO DC


Dada yetu Aisha Bwalu anawataarifu KISOMO cha kumuombea marehemu BABA yake leo jumamosi 
tarehe 27 feb 2010 kuanzia saa 9(3pm)
 address 
         19933 Stone Point Way,
          Germantown,Md,20876
            
           tafadhali zingatia muda


simu 301 792 0296
         240 821 4782

DALLAS,TEXAS EASTER PARTY

[dallas.jpg]Friday april 2,"WELCOME NIGHT" includes fashion show(African Designer)plus suprise smooth vibes Artist

Saturday Noon:soccer and basketball, and kids games,

Evening:hang out/mingling time.

night is party time which includes atleast three artists performing live a few of their songs,you gonna be dancing till dawn!!

Sunday noon:BBQ in a park and Later clubbing till dawn

Nyakati za baridi ughaibuni

Dedi Luba akiwa na bintie Zuhura wakiangalia Disney channel
Mohammed amejituliza kwenye kochi,akilalama na baridi

Vikwangua anga vyazidi kuchomoza downtown Silver Spring

pamoja snow ni mwezi sasa tangu ilipoanguka DMV,mpaka sasa ashikirimu bado imeshamiri

picha ya ashikirimu ilivyo leo Capital Heights,Maryland

Bridge ajiondoa timu ya taifa England


Mlinzi wa Manchester City Wayne Bridge amejiondoa katika kikosi cha timu ya taifa ya England na hatoichezea timu hiyo katika mashindano ya Kombe la Dunia.
Katika taarifa iliyotolewa na mawakili wake, Bridge mwenye umri wa miaka 29, amesema nafasi yake katika kikosi cha timu ya taifa ameona haitakuwa na "ufanisi na anaepusha mgawanyiko".
Mlinzi huyo wa upande wa kushoto amekuwa akitajwa kuhusiana na tuhuma za mpenzi wake wa zamani kuwa na uhusiano na John Terry.
Kocha wa England Fabio Capello mwezi huu alimvua unahodha Terry.
Katika taarifa hiyo ya Bridge iliyotolewa siku ya Alhamisi, ameongeza kusema amefikiria kwa muda mrefu nafasi yake katika kikosi cha England na hasa akihusisha matukio yaliyokuwa yakiarifiwa kwa wiki kadha.
Ameendelea kusema ni jambo la heshima kila wakati kuichezea England. Hata hivyo baada ya kufikiria kwa makini anaamini nafasi yake katika kikosi hicho kwa sasa haitakuwa na ufanisi na huenda kungesababisha mgawanyiko.

Gaddafi aitisha jihad dhidi ya Uswizi



Kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi amewataka Waislamu kuanza vita vya Jihad dhidi ya Uswizi.
Kanali Gaddafi anadai kwamba nchi hiyo imeanzisha kampeini ya kuharibu misikiti baada ya kura ya maoni nchini humo mwezi Novemba, kuidhinisha kupigwa marufuku kwa ujenzi wa minara katika misikiti ya Uswizi
Kanali Gaddafi pia ametaka waislam kote duniani kususia bidhaa za Uswizi. Kiongozi huyo wa Libya ameyasema hayo mjini Benghazi wakati wa kuadhinisha siku ya kuzaliwa kwa Mtume Mohamed.
Kumekuwa na mzozo wa kidiplomaia kati ya Libya na Uswizi tangu mwana wa Kanali Gaddafi pamoja na mkewe kukamatwa nchini humo kwa tuhuma za kumdhulumu mjakazi.
Wiki iliyopita, Libya iliwapiga marufuku raia wa muungano wa Ulaya kupata vibali vya kuzuru nchi hiyo. Hiyo ilifuatia hatua ya Uswizi kutoa orodha iliyowawekea vikwazo raia 188 wa Libya, ikiwa ni pamoja na Kanali huyo na watu wa jamii yake.

Mtoto aliyeng'ang'aniwa na madaktari afa


Maafisa nchini Brazil wanachunguza kifo cha mtoto ambaye alikuwa hajazaliwa baada ya madaktari wawili kupigana katika chumba wanapojifungua akina mama.
Vyombo vya habari nchini humo vinasema madaktari hao walikuwa waking'ang'ania kumzalisha mamake mtoto huyo.
Tayari madakatari hao wamesimamishwa kazi. Mama huyo alifanyiwa upasuaji wa dharura dakika tisini baadaye lakini mtoto akawa amefariki.

Obama ashindwa kuwashawishi wapinzani

Rais wa Marekani Barack ObamaRais Barack Obama alifanya kongamano la saa saba na wanasiasa wa Republican katika jaribio la kuwashawishi waunge mkono mpango wake wa bima ya afya.
Lakini baada ya mkutano huo wapinzani hao walisalia na msimamo ule ule. Seneta mmoja wa Republican Lamar Alexander alimweleza Rais Obama kuwa kongamano lake lilikuwa kama muuzaji wa magari anayejaribu kuuza gari lile lile lililokataliwa hapo awali.
Kufuatia msimamo huo Rais Obama amesema atalazimika kusonga mbele na mpango wake hata kama chama cha Republic kitakataa kumuunga mkono.
Rais huyo wa Marekani anapendekeza mfumo ambao utawaruhusu zaidi ya Wamarekani milioni 30 zaidi kupata Bima ya afya.
Mpango huo utagharimu serikali ya Marekani takriban dola bilioni 50 kila mwaka, kiasi ambacho warepublican wanasema ni cha juu sana kwa walipa kodi wa Marekani.

Aj Ubao


YA CHECK ME OUT ON WWW.MEXXRADIO.COM AS A SPECIAL GUEST FRIDAY FEB 26 FROM 8PM TO 10PM I WILL PLAY MY NEW 2TRACKS 4 THA FIRST TIME SO YA DONT MISS THIS STAY TUNE PAMOJAH!!!

inakuaje wachezaji wa timu moja wanavaa jezi tofauti?